Monday, March 19, 2012

MACHUPPA AULA SWEDEN, APATA TIMU MPYA, MKATABA MNONO

Machuppa
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba SC na Malindi ya Zanzibar, Athumani Machuppa amejiunga na klabu ya Vasby United ya Daraja la Kwabnza Sweden akitokeas Vasalund ya Daraja la Pili.
Machuppa ameiambia bongostaz dakika kadhaa zilizopita kwamba alilazimika kufanya majaribio kwenye timu hiyo na baada ya kufuzu ndipo akapewa mkataba wa miaka mitatu.
"Maisha yanaendelea ndugu yangu, mkataba mzuri namshukuru Mungu, kinachofuata hapa ni kazi tu, naamini unaniaminia jembe lako, wewe subiri tu kuandika mabao nayofunga huku, nina ari mpya na nguvu mpya,"alisema.

HALI YA MUAMBA KIDOGO 'ALHAMDULILLAH'

HALI ya mchezaji wa Bolton Wanderers, Fabrice Muamba inaendelea vizuri na inaonyesha dalili za matumaini, wamesema madaktari, ingawa bado yupo chumba cha wagonjwa walio chini ya uangalizi maalum.

Taarifa iliyotolewa na hospitali ambayo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 amelazwa imesema: "Fabrice Muamba bado yupo kwenye chumba wagonjwa walio chini ya uangalizi maalumkatika hospitali ya London Chest, ambako leo anaonyesha dalili ndogo za kupata naduu.
"Moyo wake sasa unapiga bila msaada wa mashine na pia anazungusha miguu na mikono yake."
Lakini taarifa hiyo imesema mustakabali zaidi wa kiungo huyo bado hauwezi kutolewa.
"Bado anaumwa sana na ataendelea kuwa karibu na uangalizi na kuhudumiwa na wafanyakazi."

WAALGERIA KUTUA ALHAMISI

Abdelmaliek Ziaya mshambuliaji wa  ESS Setif
WAKATI kikosi cha timu ya soka ya Simba kinatarajiwa kuingia kambini
leo kujiandaa na mechi yake ya kombe la Shirikisho dhidi ya ES Setif
ya Algeria, wapinzani wao hao wanatarajiwa kuwasili nchini Alhamisi 
tayari kwa mchezo huo wa kwanza utakaopigwa jumapili katika dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Mwenyekiti wa Simba Alhaj Ismail Aden Rage alisema msafara wa watu 37 kutoka Algeria utafikia katika hoteli ya Durban iliyopo katikati ya jiji la Dar es Salaam. Alisema maandalizi kwa ajili ya mchezo huo yanakwenda vema ambapo kikosi cha Simba kilichopewa mapumziko ya siku moja baada ya kutoka Morogoro ilipocheza na Mtibwa Sugar ya huko na kuchanua na ushindi wa mabao 2-1, kitaingia kambini katika hoteli ya Bamba Beach iliyopo Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Rage aliongeza kuwa kikosi chake kipo katika hali nzuri na kwa siku zilizosalia kabla ya mchezo huo anaamini kocha mkuu wa timu hiyo Mserbia Milovan Cirkovic atazitumia vema kukiweka katika hali nzuri zaidi ili kuweza kushinda mechi hiyo. Mechi hiyo itakayopigwa kuanzia saa 10 kamili jioni itachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda ambapo mwamuzi wa kati atakuwa Hudu Munyemana wakati wasaidizi wake ni Felicien Kabanda, Theogene Ndagijimana na Edouard Bahizi. Kamishna wa mechi hiyo ni Felix Tangawarima kutokaZimbabwe. Timu hizo zitarejeana Algeria Aprili 6 na iwapo Simba itashinda itacheza mechi ya kwanza nyumbani Aprili 29 mwaka huu na mshindi kati ya El Ahly Shandy ya Sudan na Ferroviario de Maputo ya Msumbiji ambapo ya marudiano itachezwa kati ya Mei 11, 12 na 13 mwaka huu. Katika hatua nyingine, kiungo wa timu hiyo Rajab Isihaka amefiwa na baba yake mzazi Mzee Isihaka ambaye alikutwa na umauti huo asubuhi ya jana jijini Dar es Salaam ambapo msimba upo nyumbani kwa marehemu Mbagala Mbagala Charambe jijini Dar es Salaam huku mazishi yakitarajiwa kufanyika leo.mwisho

SEKELTI NAYE NDANI TAMASHA LA PASAKA

Sekeleti
MWIMBAJI wa muziki wa Injili kutoka Zambia, Ephraim Sekeleti Mutalange amethibitisha kushiriki tamasha la Pasaka litakalofanyika Sikukuu ya Pasaka Aprili 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ambaye ni Mkurugenzi wa Msama Promotions, waandaaji wa tamasha hilo, Sekeleti amekubali kushiriki.
Msama alisema Dar es Salaam jana kuwa mwimbaji huyo wa nyimbo za kumsifu Mungu atatua nchini akiwa na albamu zake za Acha Kulia na Mungu Mwenyewe.
Msama alizitaja baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo kuwa ni Uniongoze na Kidonge cha Yesu. Baada ya kutikisa Uwanja wa Taifa, mashambulizi mengine yatahamia kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Aprili 9 mwaka huu.
"Sekeleti ameomba mashabiki wajitokeze kwa wingi, hivyo ni nafasi nzuri kwa Watanzania kufika kumshuhudia mwimbaji huyo," alisema Msama.
Aliongeza kwamba Sekeleti atakuja nchini na waimbaji wake 10 na ataimba 'live' siku hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
Sekeleti ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili nchini Zambia, alizaliwa mwaka 1983 katika mji wa Kalulushi, Zambia. Alimaliza elimu yake ya sekondari katika Shule ya Kalulushi mwaka 2001.
Sekeleti ni mtoto wa pili kutoka mwisho kati ya watoto sita. Aliingia kwenye muziki wa injili tangu akiwa kinda huku alifundishwa kupiga kinanda na mmisionari.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu lina malengo ya kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wajane wasiojiweza.
Kiingilio katika tamasha hilo kimetengwa katika kategoria tatu na kitakuwa sh. 2,000 kwa watoto, sh. 5,000 kwa viti vya kawaida na viti maalumu sh. 10,000.
Mbali na Sekeleti, wasanii wengine wa nyimbo za Injili watakaopamba tamasha hilo ni Rebecca Malope, Rose Muhando, Christina Shusho, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Solomon Mukubwa, Anastazia Mukabwa, Atosha Kissava na kundi la Glorious Celebration.
Pia kwaya mahiri ya Kinondoni Revival inayotamba na albamu yao mpya ya Mtu wa Nne, inatarajia kutumbuiza katika tamasha la Pasaka na Mwinjilisti Faraja Ntaboba kutoka DRC.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia.
 

MASTAA 10 NA MIKOKO 10 YA BEI CHAFU BABAKE



10. Kim Kardashian – Ferrari F430
BEI:  US dola 186,925.

9. Paris Hilton – Bentley GT Continental
BEI:  US dola 285,000

8. P. Diddy – Maybach
BEI: US dola 360,000

7. David Beckham- Custom Rolls-Royce Phantom Drophe
BEI: US dola $407,000

6. Jay Leno – Mercedes SLR McLaren
BEI:  US dola 450,000

5. Nicolas Cage - Ferrari Enzo
BEI: US dola 670,000

4. Jerry Seinfeld - Porsche 959
BEI: US dola 700,000

3. Simon Cowell - Bugatti Veyron
BEI:US dola  1,700,000

2. Rapper Birdman- Bugatti Veyron
BEI: US dola 2 Million

1. Jay Z- Maybach Exelero
BEI: US dola 8,000,000