CHAMA Cha Waandishi wa Habari za Michezo
Tanzania (TASWA), kimeanza mchakato wa Tuzo kwa Wanamichezo Bora wa Tanzania
mwaka 2011.
Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando (pichani kushoto) ameiambia
BIN ZUBEIRY leo kwamba kama ilivyokuwa mwaka uliopita Kamati ya Utendaji ya
TASWA imeamua suala la mchakato wa kuwapata wanamichezo hao lifanywe na kamati
maalum nje ya Kamati ya Utendaji ya TASWA lengo ikiwa ni kupanua wigo na
kuwashirikisha wadau wengi zaidi katika jambo hili nyeti.
Kutokana na hali hiyo Kamati ya Utendaji ya
TASWA imeshateua kamati maalum ya kusimamia tuzo hiyo, ambapo kamati hiyo
ambayo tayari imeshaanza vikao vyake jijini Dar es Salaam ipo chini ya Mhariri
Mkuu wa gazeti la Spoti Starehe, Masoud Sanani, ambaye pia aliiongoza kamati
hiyo mwaka uliopita.
Kamati hiyo ya Tuzo ilikutana mara ya
mwisho hivi karibuni kwa ajili ya kupanga namna ya kuendesha tuzo hizo kwa
mwaka huu ili iwe bora zaidi ya ilivyokuwa mwaka jana.
Pamoja na mambo mengine kamati ilikubaliana
vyama vya michezo vishirikishwe kwa kuviandikia barua ili vitume majina ya
wanamichezo wao waliofanya vizuri kwa mwaka 2011.
Kutokana na hali hiyo kila chama cha
michezo kitawasilisha kwa kamati majina
matatu ya wanamichezo wake waliofanya vizuri mwaka jana kwa wanaume matatu na
wanawake matatu, ambao mmojawao atakuwa ndiye mshindi wa mchezo husika kwa
mwaka jana.
Pia kila mshindi miongoni mwa wanamichezo
hao atashiriki kuwania tuzo ya Mwanamichezo wa Bora wa Mwaka 2011. Tarehe na mahali
ambapo tuzo itafanyika itatangazwa wiki hii baada ya kumalizika vikao muhimu,
ambapo pia mdhamini wa tuzo atatajwa, ingawa TASWA inafungua mlango kwa kampuni
zaidi zijitokeze kudhamini kwa vile tuzo ya mwaka huu itakuwa ya aina yake.
Kwa hiyo wafuatao ndio wanaunda Kamati ya
TASWA ya Kusimamia Upatikanaji wa Wanamichezo Bora wa Tanzania kwa mwaka 2011,
wengi wakiwa ni wale waliokuwepo mwaka uliopita..
Mwenyekiti wa Kamati atakuwa Sanan, ambaye
ni Mhariri wa gazeti la Spotistarehe, Katibu wa kamati atakuwa Amir Mhando
ambaye ni Katibu Mkuu wa TASWA, Mshauri
wa Kamati atakuwa Juliana Yassoda ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Idara ya
Maendeleo ya Michezo. Pia Kamati itaomba Ofisa mmoja wa Baraza la Michezo la
Taifa (BMT) naye kuwa mshauri wa kamati.
Orodha kamili ya wajumbe ni
1.Amour Hassan-Mhariri Nipashe
2. Rashid Zahoro-Mhariri gazeti la Burudani
3. Alex Luambano-Clouds FM
4. Tulo Chambo-Mhariri Tanzania Daima
5. Mbonile Burton-HabariLeo
6. Chacha Maginga-TBC1
7.Frank Sanga-Mhariri Mwanaspoti
8. Michael Maurus-Super Star
9. James Range-Star TV
10.Editha Mayemba-Radio Tumaini
11. Said Kilumanga-Chanel Ten/Magic Radio
12.Rehule Nyaulawa-Mkurugenzi Times FM
13. Angel Akilimali-Meneja Vipindi Radio
Uhuru
14. Masoud Sanan-Mhariri Spotistarehe
15. Amir Mhando-Katibu Mkuu TASWA
16. George John –Katibu Msiadizi TASWA
17.Patrick Nyembela-EATV
18: Juliana Yassoda-Naibu Mkurugenzi Idara
ya Michezo
19. Luqman Maloto-Championi
20. Deo Rweyunga-Radio One
21. Andrew Kingamkono-Mhariri Mwananchi
22. Dominick Isiji-The African
23. Ofisa kutoka BMT
0 comments:
Post a Comment