• HABARI MPYA

    Saturday, May 12, 2012

    RACHEL KUZIKWA JUMATATU GOBA


    ALIYEKUWA Mhariri wa michezo wa gazeti la Mtanzania marehemu Rachel Mwiligwa anatarajiwa kuzikwa keshokutwa (jumatatu) nyumbani kwao Goba. Marehemu aliyekutwa na umauti huo usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Mwananyamala alipolazwa kwa ugonjwa wa Nimonia, awali ilipangwa azikwe katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Katika hatua nyingine, kampuni ya BigRight Promotion kupitia kwa mkurugenzi wake Ibrahim Kamwe imepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu).kwa niaba ya mabondia,makocha na mapromota wa masumbwi nchini tunawataka familia ya rachel na kampuni ya New habari wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba. Tunatoa POLE! - MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU RACHEL PEPONI - "ameeein"


    SOURCE: DINA ISMAIL (http/mamapipito.blogspot.com)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RACHEL KUZIKWA JUMATATU GOBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top