Edward Christopher aliyepunga mikono akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la pili |
Na Mahmoud Zubeiry
SIMBA SC imetinga Fainali
ya michuano ya BankABC Sup8R baada ya kuifunga Azam FC, mabao 2-1 kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam na Jumamosi itamenyana na Mtibwa Sugar, ambayo katika
mechi ya kwanza imeifunga Jamhuri ya Pemba mabao 5-1, uwanja huo huo.
Hadi mapumziko, Simba inayotumia
wachezaji wake wa kikosi cha pili, Simba B, kinachofundishwa na Suleiman Matola,
walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na Rashid Ismail aliyeunganisha
krosi ya Edward Christopher dakika ya pili tu ya mchezo huo.
Kipindi cha pili ‘Watoto
wa Matola’ walirudi na moto na kulisakama kama nyuki lango la Azam,
wakigongeana pasi za uhakika ndefu na fupi na kuwafunika kabisa mabingwa wa
Kombe la Mapinduzi.
Christopher Edward
aliifungia Simba bao la pili kwa penalti dakika ya 56, baada ya yeye mwenyewe
kuangushwa ndani ya eneo la hatari na Luckson Kakolaki.
Azam walipata bao la
kufutia machozi dakika ya 71, mfungaji Zahor Pazi aliyeingia kipindi cha pili
kuchukua nafasi ya Gaudence Mwaikimba, baada ya kutokea purukushani kwenye
lango la Simba B.
Ushindi huu wa Simba B ni sawa na kuwalipia kisasi kaka zao, Simba A ambao walifungwa na Azam 3-0 katika Robo Fainali ya Kombe la Kagame mwezi uliopita.
Katika mchezo huo,
kikosi cha Smba kilikuwa; Abuu Hashimu(18), Miraj Adam (19), Omary Salum (11)/William
Lucian ‘Gallas’, Hassan Isihaka (5), Hassan Hatibu (15) Said Ndemla (13),
Haroun Athumani (7), Abdallah Seseme (17), Rashid Ismail (8), Edward
Christopher (9)/Ramadhan Mzee na Frank Sekule (4)Ibrahim Ajibu.
Benchi; Saleh Malande
(1), Ramadhan Mzee (2), William Lucian ‘Gallas’(3), Kenny Alex (12), Mohamed
Salum (16), Ibrahim Ajibu (20) na Jesse Nyambo (14).
Kocha; Suleiman
Matola. Msaidizi; Amri Said.
Azam FC; Wandwi
Jackson (18), Ibrahim Shikanda (21), Samir Hajji Nuhu (11), Said Mourad (15),
Luckson Kakolaki (5), Abdulhalim Humud (24), Sunday Frank (12), Jabir Aziz (25)/Khamis
Mcha, Gaudence Mwaikimba (17)/Zahor Pazi, Abdi Kassim (20) na Kipre Herman
Tcheche (27)Hamisi Mcha.
Benchi; Aishi Mfula
(1), Omary Mtaki (2), Himid Mao (23), Khamis Mcha (22), Kelvin Friday (28).
Abdulghani Gullam (14) na Zahor Pazi (9).
Kocha; Boris Bunjak
(Serbia). Msaidizi; Vivek Nagul (India).
Katika mchezo wa
kwanza, Mtibwa Sugar ilitinga Fainali kwa kishindo, kwa kuinyuka Jamhuri ya
Pemba, mabao 5-1, ambayo yalitiwa kimiani na Babu Ally Seif dakika ya 15,
Salvartoy Ntebe dakika ya 17, Mfaume Shaaban aliyejifunga dakika ya 38, Vincent
Barnabas dakika ya 43 na Awadh Juma dakika ya 85 wakati la kufutia machozi la
Jamhuri lilifungwa na Mbarouk Chande dakika ya 62.
Raha ya Ushindi SImba SC |
Kisiga Shaaban 'Malone' wa Mtibwa akikokota mpira katika mechi ya kwanza |
0 comments:
Post a Comment