• HABARI MPYA

    Friday, October 12, 2012

    KIM POULSEN AENDEA KUANGALIA VIPAJI ZANZIBAR

    Kim Poulsen

    Na Ally Mohamed, Zanzibar
    KOCHA Mkuu wa timu ya soka taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mdenmark Kim Poulsen anatarijia kuwasili visiwani Zanzibar kwa ziara maalum kwa ajili ya kuangalia mechi za Ligi Kuu ya Zanzibar inayoendelea, ili kupata wachezaji ambao atawateua katika kikosi cha Taifa Stars.
    Akizungumza kwa njia ya simu, mjumbe wa Kamati tendaji wa Zfa Taifa, Masoud Atai, amesema kuwa wamepokea taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) ya ujio wa kocha huyo.
    "Tumepokea taaifa kutoka kwa wenzetu TFF, na barua wametuletea kwamba kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars atakuja Zanzibar kwa lengo la kuangalia mechi za ligi kuu ya Zanzibar na kutizama wachezaji ambao watamfaa katika timu yake ya Taifa Stars". Alisema Atai.
    Kwa mujibu wa taarifa ya mjumbe huyo ni kuwa Kim Poulsen anatarajiwa kuwasili visiwani Zanzibar tarehe 18 ya mwezi huu na anatarajiwa kwenda kisiwani Pemba tarehe 19 ya mwezi huu na kukaa huko kwa muda wa siku 3 kwa ajili ya kuangalia mechi za ligi kuu zitakazochezwa katika kiwanja cha Gombani.
    Kim Poulsen atarejea kisiwani Unguja siku ya tarehe 22 ya mwezi huu kwa ajili ya kuangalia mechi za ligi kuu katika uwanja wa Amaan. na anatarajiwa kuondoka visiwani Zanzibar tarehe 26 ya mwezi huu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KIM POULSEN AENDEA KUANGALIA VIPAJI ZANZIBAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top