• HABARI MPYA

    Friday, October 19, 2012

    MTANZANIA KUKIPIGA MAREKANI


    Na Prince Akbar
    MTANZANIA Millan Mbise ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), itakayomwezesha kucheza mpira wa miguu nchini Marekani.
    Boniface Wambura, Ofisa Habari wa TFF, amesema Shirikisho la Soka Marekani (USSF) limemuombea hati hiyo Mbise kama mchezaji wa ridhaa ili ajiunge na timu ya Virginia Youth Soccer.
    Wambura amesema klabu ya zamani ya Mbise aliyezaliwa Agosti 18, 1994 imetajwa kuwa Super Sport FC, na mechi ya mwisho kwenye timu hiyo alicheza Novemba 15 mwaka juzi.
    Amesema TFF inafanya mawasiliano na pande husika kabla ya kutoa hati hiyo kwa mchezaji huyo kama ilivyoombwa na shirikisho hilo la Marekani.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MTANZANIA KUKIPIGA MAREKANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top