• HABARI MPYA

    Wednesday, November 21, 2012

    DI MATTEO ATUPIWA VIRAGO CHELSEA

    Di Matteo amebaki historia Chelsea

    BILIONEA Mrusi Roman Abramovich amemfukuza kazi Kocha Mtaliano, Roberto Di Matteo asubuhi ya leo baada ya matokeo mabaya mfululizo.
    Mmiliki huyo wa Chelsea, amekasirishwa na matokeo mabaya ya timu hiyo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, na kumfukuza kazi Mtaliano huyo baada ya timu kuzabwa mabao 3-0 na Juventus jana, ikiwa ni miezi sita tu tangu aipe timu hiyo taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
    Sasa mtu wa kwanza kabisa ambaye Abramovich anamtaka akarithi mikoba ya Mtaliano huyo ni kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola, na kama akikwama kwa Mspanyola huyo ambaye amesema hataki ukocha tena kwa sasa, basi atahamishia ndoana zake kwa Rafa Benitez.

    MAKOCHA WALIODUMU MUDA MFUPI CHESLEA:
    Guus Hiddink         Siku 105
    Felipe Scolari         Siku 223
    Avram Grand          Siku 247
    Andre Villas-Boas   Siku 256
    Roberto Di Matteo   Siku 262

    MATOKEO YALIYOMFUKUZISHA KAZI DI MATTEO:
    Oktoba 23: Shakhtar 2 Chelsea 1        (Ligi ya Mabingwa)
    Oktoba 28: Chelsea 2 Man United 3    (Ligi Kuu)
    Oktoba 31: Chelsea 5 Man United 4    (Kombe la Ligi)
    Novemba 3: Swansea 1 Chelsea 1      (Ligi Kuu)
    Novemba 7: Chelsea 3 Shakhtar 2      (Ligi ya Mabingwa)
    Novemba 11: Chelsea 1 Liverpool 1     (Ligi Kuu)
    Novemba 17: West Brom 2 Chelsea 1  (Ligi Kuu)
    Novemba 20: Juventus 3 Chelsea 0     (Ligi ya Mabingwa)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: DI MATTEO ATUPIWA VIRAGO CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top