// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KILI STARS KUTINGA ROBO FAINALI LEO TUSKER CHALLENGE? - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KILI STARS KUTINGA ROBO FAINALI LEO TUSKER CHALLENGE? - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Wednesday, November 28, 2012

        KILI STARS KUTINGA ROBO FAINALI LEO TUSKER CHALLENGE?

        Kim Poulsen kulia akijadiliana jambo na Msaidizi wake, Sylvester Marsh  jana, wakati wakishuhudia mechi kati ya Uganda na Ethiopia

        Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
        MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge 2012 inatarajiwa kuendelea leo kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole wakati timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars itakapojitupa dimbani kumenyana na Burundi, Int’hamba Murugamba.
        Stars, inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, inahitaji ushindi katika mchezo wa leo utakaoanza saa 12:00 jioni, ili kujihakikishia kutinga Robo Fainali, baada ya awali kushinda mabao 2-0 dhidi ya Sudan.
        Stars itamenyana na Burundi, ambayo inaongoza Kundi B kwa wastani wa mabao, japokuwa inalingana kwa pointi na Bara. Kabla ya mechi hiyo, Somalia wanaoshika mkia katika kundi hilo, watamenyana na Sudan kuanzia saa 10:00 jioni.
        Kocha wa Kilimanjaro Stars, Mdenmark Kim Poulsen amesema kwamba uwezo wa timu yake unazidi kukua siku hadi siku na sasa ana matumaini ya kufanya vizuri zaidi katika michuano hii.
        “Tuliwafunga Kenya (mchezo wa kirafiki Mwanza), tumewafunga Sudan, timu zote nzuri, Sudan wapo juu yetu kiuwezo katika viwango vya FIFA. Kwangu siangalii sana viwango vya FIFA, mpira ni pale unapokuwa uwanjani,”alisema Poulsen.
        Akilizungumzia kundi lake, B lenye timu za Sudan, Somalia na Burundi, alisema ni gumu na wanatakiwa kupambana ili kufika mbali.
        Lakini Poulsen amesema bado anawahitaji mno washambuliaji Mbwana Ally Samatta na Thomas Emanuel Ulimwengu wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) , ambao wamezuiwa na klabu yao.
        Kim alisema jitihada za kuwaomba Mazembe wawaruhusu wachezaji hao zinaendelea.
        “Sijui itakuwaje wasipokuja, itanibidi tu niwatumie wachezaji hawa hawa waliopo, najua nina mshambuliaji mmoja, lakini nitawatumia hawa hawa waliopo, Simon Msuva anaweza akawa mshambuliaji, nitafanyeje,”.
        “Siwezi kuita mchezaji mwingine kutoka nyumbani kwa sasa, kwa sababu mtu lazima umuone uwezo wake, huwezi kumuita tu, kwa hivyo naomba Mungu tu Samatta na Ulimwengu waje,”alisema Kim.
        Katika mchezo wa leo, Kim ambaye amekuwa akifuatilia kwa makini mashindano haya ili kujua uwezo wa timu zote, hatarajiwi kuwa na mabadiliko kwenye kikosi chake kutoka kile kilichoifunga Sudan 2-0.
        Kama kawaida, Nahodha Juma Kaseja anatarajiwa kuanza, kulia akicheza Erasto Nyoni, kushoto Amir Maftah na mabeki wa kati, Kevin Yondan na Shomary Kapombe. Kiungo mkabaji Frank Domayo, wingi ya kulia Simon Msuva, kushoto Mrisho Ngassa kiungo mchezeshaji Salum Abubakar na Mwinyi Kazimoto atacheza nyuma ya mshambuliaji pekee, John Bocco ‘Adebayor’.
        Mfumo wa sasa Kim unaonekana kuwa na tija kwa Stars, kwani analundika viungo wengi, huku akitumia mawinga ambao wanasababisha presha kubwa ya mashambulizi.
        Leo kama Bocco atakuwa makini anaweza kufunga zaidi ya mabao mawili aliyofunga kwenye mchezo wa kwanza, kwani kama alivyosema timu inazidi kuimarika siku hadi siku.

        MSIMAMO KUNDI A:
                              P   W  D   L    GF GA GD Pts
        Uganda          2    2    0    0    2    0    2    6
        Kenya            2    1    0    1    2    1    1    3
        Ethiopia         2    1    0    1    1    1    0    3
        Sudan Kusini 2    0    0    2    0    3    -3   0

        MSIMAMO KUNDI B: 
                              P   W  D   L    GF GA GD Pts
        Burundi         1    1    0    0    5    1    4    3
        Tanzania       1    1    0    0    2    0    2    3
        Sudan           1    0    0    1    0    2    -2  0
        Somalia         1    0    0    1    1    5    -4  0

        MSIMAMO KUNDI C:
                             P   W  D   L    GF GA GD Pts
        Rwanda        1    1    0    0    2    0    2    3
        Eritrea           1    0    1    0    0    0    0    1
        Zanzibar        1    0    1    0    0    0    0    1
        Malawi           1    0    0    1    0    2    -2   0

        VIWANGO VYA UBORA FIFA
        NCHI                 NAFASI
        Uganda             86
        Malawi              101
        Ethiopia            102
        Sudan               102
        Rwanda             122
        Burundi             128
        Kenya               130
        Tanzania           134
        Zanzibar            134
        Somalia             193
        Eritrea               192
        Sudan Kusini     200
        (Viwango hivi vimetoka mwezi huu)
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: KILI STARS KUTINGA ROBO FAINALI LEO TUSKER CHALLENGE? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry