Profesa Milovan baada ya kuibuka Taifa |
Kocha aliyetimuliwa Simba SC, Profesa Milovan Cirkovick raia wa Serbia, jana aliibuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Tanzania na Cameroon na kuteka hadhira.
Profesa Milovan aliwapungia mkono mashabiki wa Simba ambao walimjibu kwa shangwe zito.
baadaye Milovan, aliwasalimia baadhi ya wadau na kwenda kuketi kushuhudia mchezo huo. Wakati wa mapumziko, alikwenda kusalimiana na kocha aliyerithi nafasi yake, Mfaransa Patrick Liewig. Tabiri nini kinakuja, haswa katika wakati huu ambao Liewig ameingia kwenye mgogoro na wachezaji mafaza Simba SC?
Milo akiwaangalia mashabiki wa Simba |
Milo amemtia mikononi Liewig |
Milo kama Check Norris |
Achana naye Babu Mikogo, mzee kijana |
Anampa 'Hi' Babu Mfaransa |