• HABARI MPYA

    Thursday, April 04, 2013

    3-0 MADRID YAWATANDIKA AKINA DROGBA NA SNEIJDER


    KLABU ya Real Madrid imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya usiku wa jana kuilaza Galatasaray mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Bernabeu.
    Cristiano Ronaldo alifunga bao la kwanza mapema kipindi cha kwanza dakika ya tisa kabla ya Karim Benzema kufunga la pili dakika ya 29. 
    Gonzalo Higuain aliyetokea benchi kipindi cha pili alifunga la tatu kwa kichwa dakika ya 73 na kuwafanya Madrid waende kwenye Uwanja wa Turk Telecom Arena Jumanne ijayo kifua mbele.
    Didier Drogba aliyeiongoza Chelsea kutwaa taji hilo la Ulaya msimu uliopita, jana alipatya nafasi mbili nzuri lakini akashindwa kuzitumia.
    Katika mchezo huo, kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Diego Lopez, Varane, Ramos, Coentrao, Khedira, Ronaldo, Ozil/Modric dk80, Alonso, Essien, Di Maria/Pepe dk86 na Benzema/Higuain dk65.
    Galatasaray: Muslera, Dany Nounkeu, Kaya, Eboue, Altintop/Bulut dk78, Inan, Felipe Melo, Riera/Amrabat dk83, Sneijder/Zan dk46, Yilmaz na Drogba.
    Katika mchezo mwingine jana, Malaga na Borussia Dortmund zilitoka sare ya bila kufungana.

    Up and over: Cristiano Ronaldo scored the first against Galatasaray at the Santiago Bernabeu
    Kitu na boksi: Cristiano Ronaldo akifunga bao la kwanza dhidi ya Galatasaray Uwanja wa Santiago Bernabeu
    Up and over: Cristiano Ronaldo scored the first against Galatasaray at the Santiago Bernabeu
    In the goals: Karim Benzema got the second for the hosts
    Karim Benzema akishangilia bao lake
    Struggle: Didier Drogba led the line for the visitors
    Malalamiko: Didier Drogba akilalamika
    Three and easy: Gonzalo Higuain scored the third with a glancing header
    La tatu kiulainiii: Gonzalo Higuain alifunga bao la tatu kwa kichwa
    Three and easy: Gonzalo Higuain scored the third with a glancing header
    Rough and tumble: Sergio Ramos (left) drags Didier Drogba to the floor in the second half
    Mpambano wa wanaume: Sergio Ramos (kushoto) akipambana na Didier Drogba kipindi cha pili jana ambaye alianguka kama anavyoonekana picha ya chini
    Rough and tumble: Sergio Ramos (left) drags Didier Drogba to the floor in the second half
    Over you go: Ronaldo hits the deck after Semih Kaya (centre) backs into the Portugal forward
    Mpiganaji: Ronaldo akipambana dhidi ya wachezaji wa Galatasaray
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: 3-0 MADRID YAWATANDIKA AKINA DROGBA NA SNEIJDER Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top