• HABARI MPYA

    Friday, May 03, 2013

    BENITEZ AWA KOCHA ENGLAND, VAN PERSIE ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA LIGI KUU 2013


    KOCHA wa Chelsea, Rafael Benitez ameshinda tuzo ya kocha bora wa mwezi April Ligi Kuu England baada ya kuiongoza timu yake kucheza mechi nne bila kufungwa, wakati mshambuliaji wa Manchester United, Robin van Persie ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora.
    Mafanikio haya yanakuja saa kadhaa baada ya kocha wa Manchester United, Alex Ferguson kusema Benitez ndiye mtu pekee anayemvutia akiwa kazini Stamford Bridge.
    Robin van Persie ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kwa mara ya pili msimu huu, baada ya kushinda pia na Desemba.
    CV filler: Rafael Benitez was voted April's Manager of the Month for the Premier League
    Mjuzi: Rafael Benitez amechaguliwa kocha bora wa April Ligi Kuu England
    Multiple winner: Robin van Persie picked up his fifth Player of the Month award
    Mkali wa wakali: Robin van Persie ameshinda tuzo ya tano ya Mchezaji Bora wa Mwezi

    TUZO ZA BENITEZ KOCHA BORA MWEZI

    Novemba 2005 - Liverpool
    Desemba 2005 - Liverpool
    Januari 2007 - Liverpool
    Oktoba 2008 - Liverpool
    Machi 2009 - Liverpool
    Aprili 2013 - Chelsea
    Mara ya mwisho kocha wa Chelsea kushinda tuzo hiyo ilikuwa ni Aprili mwaka 2011, ilipochukuliwa na Carlo Ancelotti kabla hajatupiwa virago na klabu.
    Pamoja na kukandiwa sana na mashabiki wa Chelsea, Benitez ameendelea kufanya vizuri sasa akiwania nafasi ya tatu katika Ligi Kuu na tayari ameiwezesha timu kutinga fainali ya Europa League kwa kishindo.

    WACHEZAJI BORA WA MWEZI 2012/2013 

    Steven Fletcher (Sunderland) - Septemba
    Juan Mata (Chelsea) - Oktoba
    Marouane Fellaini (Everton) - Novemba
    Robin van Persie (Man United) - Desemba
    Adam le Fonde (Reading) - Januari
    Gareth Bale (Tottenham) - Februari
    Jan Vertonghen (Tottenham) - Machi
    Robin van Persie (Man United) - Aprili
    Deadly: Van Persie's latest goal was from the penalty spot against former club Arsenal
    Muuwaji: Van Persie bao lake la mwisho alifunga kwa penalti dhidi ya klabu yake ya zamani, Arsenal

    MAKOCHA BORA WA MWEZI 2012/2013 

    David Moyes (Everton) - Septemba 2012
    Alex Ferguson (Man United) - Oktoba 2012
    Steve Clarke (West Brom) - Novemba 2012
    Andre Villas-Boas (Tottenham) - Desemba 2012
    Brian McDermott (Reading) - Januari 2013
    Andrew Villas-Boas (Tottenham) - Februari 2013
    David Moyes (Everton) - Machi 2013
    Rafael Benitez (Liverpool) - Aprili 2013  

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BENITEZ AWA KOCHA ENGLAND, VAN PERSIE ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA LIGI KUU 2013 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top