• HABARI MPYA

    Thursday, January 02, 2014

    MAN UNITED YATAKA KUSAJILI STRAIKA HATARI KINDA LA CROATIA

    KLABU ya Manchester United ipo kwenye mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Dinamo Zagreb, Robert Muric. 
    Kocha David Moyes anaweza kuwa tayari kutoa kiasi cha Pauni 300,000 kwa ajili ya kinda huyo mwenye umri wa miaka 17, licha ya kwamba mchezaji huyo anauzwa kwa Pauni Milioni 6.
    Kuna utata kama Muric amesaini Mkataba wa mchezaji wa kulipwa au la. Chelsea na Barcelona pia zimekuwa zikimtolea macho chipukizi huyo wa Croatia, aliyeng'ara katika Kombe la Dun chini ya umri wa miaka 17.

    Sokoni: David Moyes anataka kumsaini mshambuliaji kinda Robert Muric (kushoto) kutoka Dinamo Zagreb
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED YATAKA KUSAJILI STRAIKA HATARI KINDA LA CROATIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top