• HABARI MPYA

    Tuesday, April 15, 2014

    LEKJAA AWA RAIS MPYA WA SOKA MOROCCO

    Na Princess Asia, Dar es Salaam
    SHIRIKISHO la Soka Morocco limepata uongozi mpya, kufuatia Fouzi Lekjaa kuchaguliwa kuwa rais mpya wa FRMF kwa miaka minne ijayo.
    Kijana huyo umri wa miaka 43 alichaguliwa katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi uliofanyika juzi, mjini Skhirat karibu na Rabat. 
    Bado kijana; Rais mpya wa FRMF, Fouzi Lekjaa akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kushinda kiti hicho juzi

    Amerithi kiti cha Al Fassi Firhi na ataongoza kuanzia mwaka huu hadi 2018 utakapoitishwa uchaguzi mwingine.
    Uchaguzi huo ulihudhburiwa na Makamu wa pili wa Rais wa CAF, Almamy Kabele Camara na Rais wa Bodi ya Rufaa ya CAF, Prosper Abega.
    Lekjaa anakuwa Rais wa 15 kihistoria ndani ya FRMF  tangu ilipoundwa mwaka 1955.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LEKJAA AWA RAIS MPYA WA SOKA MOROCCO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top