• HABARI MPYA

    Saturday, September 13, 2014

    BALOTELLI AANZA KAZI LIVERPOOL IKIPIGWA KIDUDE NYUMBANI NA VILLA

    BAO pekee la Gabby Agbonlahor dakika ya tisa siku tatu tangu asaini Mkataba mpya wa miaka minne, limeipa Aston Villa ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya Liverpool Uwanja wa Anfield jioni ya leo.
    Hicho kinakuwa kipigo cha pili msimu huu kwa Liverpool, baada ya awali kufungwa mabao 3-1 na Manchester City Uwanja wa Etihad.
    Mshambuliaji mpya, Mario Balotelli aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka AC Milan, alichezea kwa mara ya kwanza Liverpool lakini hakuweza kuiepusha na kipigo hicho.
    Kikosi cha Liverpool kilikuwa: Mignolet, Manquillo, Lovren, Sakho, Moreno, Gerrard, Henderson, Markovic/Borini dk71, Coutinho, Lallana/Sterling dk61 na Balotelli/Lambert dk71.
    Aston Villa: Guzan, Hutton, Senderos, Baker, Cissokho, Cleverley/Sanchez dk86, Westwood, Delph, Agbonlahor/Bent dk90, Weimann/N'Zogbia dk72 na Richardson.
    Mwanzo magumu; Mshambuliaji mpya wa Liverpool, Mario Balotelli akimtoka beki wa Aston Villa leo Uwanja wa Anfield. Liverpool ililala 1-0
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALOTELLI AANZA KAZI LIVERPOOL IKIPIGWA KIDUDE NYUMBANI NA VILLA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top