Luboslav Penev amefukuzwa kazi Bulgaria |
"Tumevunja Mkataba na Penev," amesema Rais wa BFU, Borislav Mihaylov katika Mkutano na Waandishi wa Habari. "Timu haijafanya vizuri na tunakaribia kupoteza nafasi ya kufuzu kwenye Fainali za Euro 2016, pamoja na kwamba timu mbili za juu zinafuzu moja kwa moja.
"Natumai tutakuwa na kocha mpya wakati wa mwaka mpya. Naweza kukuambia kocha mpya hatakuwa mgeni,"amesema.
Penev, mwenye umri wa miaka 48, aliongeza Mkataba wa miaka miwili Novemba mwaka jana, lakini matokeo mabaya kwenye mechi za kufuzu Euro 2016 yanamuondoa kazini baada ya miaka mitatu.
Bulgaria, ambayo imeshindwa kufuzu kwenye mashindano yoyote makubwa tangu mwaka 2004, inashika nafasi ya nne katika Kundi H ikiwa na pointi nne baada ya mechi kibao, ikizidiwa pointi sita na vinara Croatia na tano na Italia na Norway.
0 comments:
Post a Comment