Bengo akishangilia bao lake |
Huo unakuwa ushindi wa tisa katika mechi 14 kwa Villa, na kukifanya kikosi cha kocha Sam Ssimbwa kiindoe KCC katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi, kwa kufikisha pointi 30, ikizidiwa moja tu na vinara, Vipers.
Kipigo hicho kinakuwa cha nne kwa timu ya Fred Kajoba, Bright Stars msimu huu, ambacho kinawafanya washuke kwa nafasi moja hadi ya nane wakibaki na pointi zao 20.
Wenyeji walipata bao la kuongoza dakika ya 17 baada ya mchezaji wa Villa kutoka Nigeria, Victor Emenayo kuchezewa rafu kwenye eneo la hatari la Bengo akaenda kufunga
0 comments:
Post a Comment