• HABARI MPYA

    Wednesday, January 28, 2015

    LUIS FIGO ATANGAZA KUGOMBEA URAIS WA FIFA MEI

    MWANASOKA wa zamani wa kimataifa wa Ureno, Luis Figo ametangaza atagombea Urais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). 
    Gwiji huyo mwenye umri wa miaka 42 anaungwa mkono na Wajumbe watano wa FIFA - kiwango cha chini kinachotakiwa ili kuingia katika uchaguzi utakaofanyika Mei.
    Figo anakuwa wa pili mwenye jina kubwa kuingia kwenye mbio za Urais wa FIFA, baada ya David Ginola kuweka wazi nia yake ya kuwania nafasi, lakini winga huyo wa zamani wa Newcastle na Tottenham bado hajapata Wajumbe watano wa kumsapoti.  
    Luis Figo announced his intention to stand for the FIFA presidency on Wednesday
    Luis Figo ametangaza nia yake ya kuwania Urais wa FIFA leo
    Figo won 127 international caps for his native Portugal and scored 32 goals
    Figo aliichezea timu yake ya taifa Ureno mechi 127 na kuifungia mabao 32 

    WASIFU WA LUIS FIGO

    Umri: Miaka 42 
    Klabu alizochezea:
    Sporting (1989–1995) - mechi 137, mabao 16
    Barcelona (1995–2000) - mechi 172, mabao 30
    Real Madrid (2000–2005) - mechi 164, mabao 38
    Inter (2005–2009)- mechi 105, mabao 9
    Mechi za kimataifa: 
    Mechi 127 Ureno, mabao 32
    Mataji na tuzo: 
    Barcelona - La Liga mawili, Copa del Reys mbili, Kombe la Washindi la UEFA moja, UEFA Super Cup moja,
    Real Madrid - La Liga mawili, Ligi ya Mabingwa moja, UEFA Super Cup moja
    Inter Milan - Serie A manne, Coppa Italia moja
    Tuzo binafsi: 
    Mwanasoka Bora wa Ureno kuanzia 1995 hadi 2000
    Ballon d'Or mwaka 2000
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LUIS FIGO ATANGAZA KUGOMBEA URAIS WA FIFA MEI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top