BINGWA asiyepingika wa zamani wa dunia uzito wa juu, Lennox Lewis amesema Floyd Mayweather ni mtaalamu mkubwa wa ngumi.
"Watu wengine wanataka kuona damu, wanachukizwa wasipoziona. Lakini haiondoi ukweli kwamba Floyd ni mtaalamu mkubwa,"amesema Muingereza huyo.
"Watu wengine wanataka kuona damu, wanachukizwa wasipoziona. Lakini haiondoi ukweli kwamba Floyd ni mtaalamu mkubwa,"amesema Muingereza huyo.
Akizungumzia uwezekano wa pambano la Amir Khan na Mayweather, anasema; "Khan ni bondia, anatembea vizuri miguu yake. Kitu pekee ambacho Khan hana ni uzoefu mkubwa na ninahisi kwamba anaweza,"amesema Lewis.
Bingwa mwingine wa zamani wa uzito wa juu, David Haye amemtetea Mayweather. "Sanaa ya ngumi ni kupiga bila kupigwa. Mapambano 48 bila kupoteza kwa Money ni uthibitisho wa ubora wake,"amesema.
Haye amesema pambano la marudiano baina ya waili linaweza kutokea na ndilo litamaliza ubishi.
0 comments:
Post a Comment