• HABARI MPYA

    Sunday, May 03, 2015

    MAYWEATHER ASHINDA KWA POINTI DHIDI YA PACQUIAO

    RAUNDI KWA RAUNDI 
    Mayweather Raundi Pacquiao 
              101        9
               92       10
               93       10
               9       10
              105        9
               9       10
              10        9
              108        9
              109       10
               910       10
              1011         9
              1012        10
             115JUMLA       115
    BONDIA Floyd Mayweather amekamilisha pambano lake la 48 bila kupoteza, akishinda yote baada ya kumshinda kwa pointi Mfilipino, Manny Pacquiao.
    Katika pambano hilo lililofanyika ukumbi wa MGM Granc mjini Las Vegas, Mmarekani huyo ameshinda kwa pointi za majaji wote, 118-110, 116-112 na 116-112.
    Mayweather sasa ni bingwa wa dunia asiyepingika katika uzito wa Welter na mmiliki wa mataji yote makubwa, WBA, WBO na WBA.
    Tofauti na ilivyotarajiwa, Pacquiao hakuweza kurusha ngumi nyingi kutokana na mpinzani wake kuhama hama ulingoni.
    Mayweather aliitumia vizuri staili yake ya kupigana kwenye kona na kufanikiwa kumtupia ngumi nyingi za kudonoa mpinzani wake kuanzia mwanzo hadi mwisho.
    Kufika raundi ya 11, tayari mwelekeo wa pambano ulianza kuonekana ‘Mtu Pesa’ atashinda- ingawa Man Pac alikuwa anashangiliwa zaidi ukumbini.
    Mayweather alistahili ushindi na alionyesha yeye ni bondia bora wa kizazi cha sasa.
    Mayweather made contact with a straight right - a weapon he kept deploying against Pacquiao

    Mayweather akimrushia konde mpinzani wake Pacquiao katika pambano lao lililomalizika hivi karibuni

    PICHA ZAIDI NENDA: 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAYWEATHER ASHINDA KWA POINTI DHIDI YA PACQUIAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top