• HABARI MPYA

    Sunday, May 03, 2015

    RONALDOOO, HUYU MTU WEKA MBALI NA WANYONGE, APIGA ZOTE TATU REAL IKITAKATA LA LIGA

    MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amefunga hat-trick yake ya 29 tangu aanze kuchezea Real Madrid katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Sevilla katika La Liga usiku huu.
    Ushindi huo unaifanya Real ifikishe pointi 85 na kupunguza pengo la pointi inazozidiwa na Barcelona hadi kubaki mbili baada ya timu zote kucheza mechi 35.
    Hii inakuwa mara ya kwanza timu ya Unai Emery inafungwa nyumbani baada ya mechi 35 na ni Ronaldo anayevunja rekodi ya timu hiyo kucheza mechi 15 bila kufungwa.
    Ronaldo alifunga mabao hayo katika dakika za 36, 37 na 69 Uwanja wa Ramon Sanchez Pizjuan, wakati mabao ya Bacca kwa penalti dakika ya 45 na Iborrs dakika ya 79. 
    Cristiano Ronaldo led Real Madrid to victory and scored twice for his team in the first half of the game
    Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid mabao yote katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Sevilla

    PICHA ZAIDI NENDA: 

    http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-3065612/Sevilla-2-3-Real-Madrid-Cristiano-Ronaldo-continues-formidable-scoring-form-Ramon-Sanchez-stadium-hat-trick.html#ixzz3Z1AyyIWA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDOOO, HUYU MTU WEKA MBALI NA WANYONGE, APIGA ZOTE TATU REAL IKITAKATA LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top