• HABARI MPYA

    Friday, May 11, 2012

    NESTA ABWAGA MANYANGA AC MILAN BAADA YA MIAKA 10 YA MAFANIKIO


    Alessandro Nesta - Milan
    Getty
    BEKI wa AC Milan, Alessandro Nesta ametangaza kuondoka kwenye klabu hiyo mwishoni mwa msimu na kwenda kucheza nje ya Ulaya, Marekani ikipewa kipaumbele.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 36 anayecheza beki ya kati, ambaye mkataba wake Milan unaisha Juni, atakamilisha miaka 10 ya kuwatumikia The Rossoneri, aliojiunga nao akitokea Lazio mwaka 2002 kwa dau la euro Milioni 30.5.
    Amekuwa akihusishwa na mpango wa kuhamia Juventus, lakini amesema kwamba hatacheza tena Ulaya kutokana na kuamini hatamudu tena kasi ya soka ya Ulaya kwa umri wake.
    "Soka ya Italia na Ulaya ni ya kasi sana hivi sasa kwangu," alisema kwenye mkutano na Waandishi wa Habari. "Kama sitaona muhimu, ni bora nibaki nyumbani.
    "Nimeshinda vitu vingi sana, lakini kwa heshima kwa klabu na wachezaji wenzangu, nimeamua kujaribu uzoefu mwingine katika klabu ambayo nitaweza kufanya vizuri."
    Tangu awasili San Siro, Nesta ameisaidia Milan kutwaa mataji mawili ya Serie A na mawili ya Ligi ya Mabingwa na mengineyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NESTA ABWAGA MANYANGA AC MILAN BAADA YA MIAKA 10 YA MAFANIKIO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top