• HABARI MPYA

    Saturday, April 11, 2015

    COASTAL YAZINDUKA, YAICHAPA JKT 2-0, BIN SLUM ACHEZA KIDUKU JUKWAANI CHAMAZI

    Nassor Bin Slum (katikati) akicheza kiduku kushangilia ushindi wa Coastal Union leo Chamazi
    COASTAL Union imeshinda mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na mfadhili wa timu hiyo aliyerejea wiki iliyopita, Nassor Bin Slum akacheza kiduku jukwaani.
    Ikitoka kufungwa mabao 8-0 na Yanga SC, Coastal leo ilikuwa timu tofauti Chamazi, ikicheza soka maridadi na kupata ushindi muhimu wa ugenini.
    Mabao ya Coastal yamefungwa na Rama Salim na Iker Obinna na sasa mabingwa hao wa Ligi Kuu 1988 wanafikisha pointi 27 baada ya kucheza mechi 23 na wanapanda hadi nafasi ya sita kutoka ya 11 kwenye msimamo wa ligi hiyo.
    Bin Slum alitangaza kurejea Coastal mapema wiki hii kufuatia matokeo mabaya mfululizo kiasi cha kuibuka hofu ya kushuka daraja, lakini bahati mbaya, mchezo wa kwanza, timu hiyo ikalala 8-0 kutoka Yanga SC kabla ya kuzinduka leo.
    Leo Bin Slum alikuwa mwenye furaha jukwaani, akiwa amejichanganya na mashabiki wakicheza ‘viduku’ kushangilia mabao na soka ‘iliyoshiba’.
    Katika mechi nyingine za ligi hiyo leo, Azam FC imetoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro, Ndanda imetoka sare ya 0-0 na Prisons Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara wakati mchezo kati ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting uliokuwa uchezwe leo Shinyanga, umesogezwa mbele hadi Jumatatu.
    Bin Slum a pili kushoto akiwa na manazi wenzake wa Coastal Chamazi leo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: COASTAL YAZINDUKA, YAICHAPA JKT 2-0, BIN SLUM ACHEZA KIDUKU JUKWAANI CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top