![]() |
Marehemu Kanumba |
Mdogo wa marehemu, Seth Bosco alitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu kifo hicho, lakini zilitofautiana huku pia kukiwa na taarifa ya Polisi wa Mkoa wa Kinondoni.
Kauli mbili tofauti za Seth
Alipohojiwa na waandishi wa habari, Jumamosi asubuhi, Seth alisema Kanumba alifika nyumbani akiwa na Lulu saa sita usiku wa kuamkia siku hiyo wakiwa wanazozana wakaingia chumbani lakini hazikupita dakika tatu, Lulu akatoka na kumfuata Seth na kumwambia Kanumba amejipigiza ukutani amedondoka chini.
Seth alisema alikwenda na kumkuta Kanumba akiwa chini huku povu likimtoka mdomoni akampigia daktari simu, ambapo baada ya kumpima, daktari huyo akashauri apelekwe Hospitali Muhimbili.
Seth anasema wakati anakwenda hospitali alimwacha Lulu nyumbani na aliporudi hakumkuta na hajui alishikwa vipi na polisi.
Akihojiwa na vyombo vya habari mchana huo wa Jumamosi, Seth anasema baada ya kula chakula cha jioni, Kanumba alimwambia ajiandae waende klabu.
Seth anasema alimwambia Kanumba kuwa tayari amejiandaa, Kanumba akasema nisubiri. Kanumba akaingia chumbani, ghafla akasikia mlio wa gari, Lulu akashuka na kuingia ndani, akapitiliza moja kwa moja chumbani kwa Kanumba, baada ya muda mfupi, Seth akasikia mzozo chumbani, akaona kimya.
Lulu akatoka akiomba msaada kwa Seth kuwa Kanumba kaanguka, aliingia akamkuta akiwa amelala chini hivyo akampigia simu daktari.
Akasema wakiwa njiani wakapitia Kituo cha Polisi cha Oysterbay wakiwa na Lulu, baada ya maelezo, polisi wakamwambia Lulu abakie kwa ajili ya maelezo zaidi.
Maswali ya kujiuliza
1. Kwa mujibu wa Kamanda Kenyela kifo hicho kilitokea saa 9 usiku, Je, Kanumba alimwambia mdogo wake wajiandae kwenda klabu muda huo?
2. Seth amezungumza kauli mbili tofauti za tukio hilo. Je, ipi ni taarifa sahihi?
3. Ni saa ngapi Seth na Kanumba walikuwa wanapata chakula cha jioni?
4. Kanumba alikuwa amerudi akitokea klabu au ndiyo alikuwa anataka kwenda klabu?
5. Hivi karibuni, Lulu alikaririwa na vyombo vya habari akisema hana mpenzi. Je, Kanumba alikuwa mpenzi wake?
6. Siku zote Kanumba alikuwa akidai hatumii kilevi chochote. Je, ni nani alikuwa anakunywa Jack Daniel's chumbani?
7. Je, Lulu alikimbia baada ya kifo cha Kanumba au aliambatana na Seth kwenda Muhimbili kabla ya Polisi kumshikilia katika kituo cha Oysterbay walipokwenda kufuata PF3?
8. Je, Lulu na Kanumba waliingia pamoja nyumbani kwa Kanumba au Lulu alikuja baadaye?
9. Lulu alikuwa anazungumza na nani kwenye simu na ni nini kilikuwa kinazungumzwa?
10. Lulu alikamatwa na polisi akiwa wapi?
0 comments:
Post a Comment