• HABARI MPYA

    Tuesday, April 17, 2012

    MFALME WA MABAO ITALI ATUNGIKA DALUGA, KISA KIFO CHA MCHEZAJI MWENZAKE JUMAMOSI

    Di Natale
    NAHODHA wa Udinese ya Italia, Antonio Di Natale amesemja anaweza kustaafu mwishoni mwa msimu, kufuatia kifo cha mchezaji mwenzake wa zamani, Piermario Morosini akiichezea Livorno Jumamosi.
    Kijana wa umri wa miaka 25, Morosini, ambaye alikuwa akicheza kwa mkopo kutoka klabu hiyo ya Serie A, Udinese, alizimia na kufariki dunia baada ya kupata tatizo la moyo katika mechi ya Serie B huko Pescara.
    Jana, Di Natale alisema soka inachezwa sana Italia na kwa hilo; ''mwaka jana nilifikiria kustaafu. ... nitacheza hizo mechi sita za mwisho kwa Mario na kasha tutaona.''
    Di Natale ana umri wa miaka 34. Mshambuliaji huyo wa Itali amekuwa mfungaji bora wa Serie A kwa misimu  miwili iliyopita.
    Kwa sasa anashika nafasi ya pili kwa mabao yake 20, akizidiwa matatu tu na Zlatan Ibrahimovic wa AC Milan.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MFALME WA MABAO ITALI ATUNGIKA DALUGA, KISA KIFO CHA MCHEZAJI MWENZAKE JUMAMOSI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top