![]() |
Walcott katikati ya Song kulia na Sagna kushoto |
MUINGEREZA Theo Walcott amesema
kwamba Arsenal ilianza ligi rasmi msimu huu baada ya kuifunga 5-3 Chelsea, Oktoba
29, mwaka jana.
Ushindi huo ulikuja baada ya
Arsenal kuuanza msimu vibaya ikiwemo kutandikwa mabao 8-2 na Manchester United.
Walcott alicheza kwa kikubwa
sana siku hiyo akiwa na jezi ya Arsenal kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, na
akafunga bonge la bao lililodhihirisha kipaji na umahiri wake.
Dogo huyo wa umri wa miaka 23
amezungumzia mechi hiyo kama moja ya mechi ambazo hawezi kuzisahau msimu huu na
ndiyo iliyowafufua.
"Mechi na Chelsea ilikuwa
hatua kubwa kwa sababu tulijua tuko vizuri [wakati huo]," alisema Walcott.
"Kwenda nje ya nyumbani na
kufunga mabao mengi, ilikuwa ni kila kitu. Ilikuwa babu kubwa jinsi
tulivyoshirikiana, baada ya mechi (furaha yake) ilikuwa kama tumetwaa ubingwa
wa Ligi Kuu.
"Huo ni moja ya wakati
ambao tunataka utokee tena na bahati nzuri umetokea tena katika wiki za
karibuni."
Walcott amefunga mabao manane
katika timu yake hadi sasa msimu huu, mawili kati ya hayo alifunga kwenye
ushindi wa 5-2 dhidi ya Spurs, Februari.
0 comments:
Post a Comment