• HABARI MPYA

    Sunday, April 15, 2012

    CHELSEA YATUMA SALAMU BARCA, YAUA 5-1 NA KUTINGA FAINALI FA

    Didier Drogba (wa tatu kushoto) akishangilia na wachezaji wenzake baada ya kufunga kwenye Uwanja wa Wembley, London leo. Chelsea ikishinda 5-1 dhidi ya Spurs Nusu fainali ya FA
    KLABU ya Chelsea usiku huu imeitandika Tottenham Hotspur mabao 5-1 kwenye Uwanja wa Wembley na kutinga fainali ya Kombe la FA ambako itamenyana na Liverpool.
    Shukrani kwao Didier Drogba, Juan Mata, Ramires, Frank Lampard na Florent Malouda waliofunga mabao hayo, yanayoiwezesha Chelsea kucheza fainali ya nne ya Kombe la FA ndani ya miaka sita.
    Bao pekee la Tottenham lilifungwa na Gareth Bale.
    Ushindi huo unakuja wakati Chelsea inaelekea kwenye mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Barcelona Uwanja wa nyumbani, Stamford Bridge Jumatano.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YATUMA SALAMU BARCA, YAUA 5-1 NA KUTINGA FAINALI FA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top