![]() |
Abidal |
KOCHA wa Barcelona, Pep
Guardiola amemtembelea beki Eric Abidal hospitali jana baada ya mchezaji huyo
kufanyiwa upasuaji wa ini mapema wiki hii.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa
Ufaransa amepigwa kisu na inasemekana anaendelea vizuri baada ya zoezi hilo
gumu.
Guardiola alitumia muda wa
dakika 20 akiwa na Abidal na familia yake, na amemtakia mchezaji huyo kupona
haraka katika upasuaji huo wa pili juu ya tatizo hilo.
Rais wa Barcelona, Sandro Rosell
alisema kwamba Mfaransa huyo anaendelea vizuri.
0 comments:
Post a Comment