• HABARI MPYA

    Monday, April 16, 2012

    LAMPARD: TUTAKOMAA NAO NA MESSI WAO

    Lampard
    KIUNGO wa Chelsea, Frank Lampard amesema kwamba kuifunga Barcelona katika mechi ya kwanza ya Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa Jumatano itakuwa changamoto kubwa zaidi katika maisha yake soka.
    Lampard amekutana na Barca mara kadhaa na pia amecheza dhidi ya timu nyingine nyingi kubwa Ulaya katika maisha yake ya soka, lakini anaamini timu hiyo ya Hispania kwa sasa inatisha na atakuwana na timu bora zaidi tangu aanze soka.
    Wachambuzi wengi wanaipa nafasi timu ya Pep Guardiola kuingia fainali itakayochezwa mjini Munich na pia Lampard anazimikia vipaji vya wachezaji wa wapinzani hao kama Lionel Messi, Xavi na Andres Iniesta.
    Chelsea inajiandaa kwa mechi ya kesho Uwanja wa Stamford Bridge ikitoka kushinda 5-1 dhidi ya Tottenham katika Nusu Fainali ya Kombe la FA Uwanja wa Wembley, lakini Lampard amesema hakuna kulala hata kidogo katika usiku watakaoivaa timu bora, Barca.
    "Nafahamu watu wanasema sisi ni ‘wahanga’ kwa sababu kila mmoja anahisi Barcelona anaweza kupita kwa kila mmoja. Ni sawa, kuwa na mchezaji kama (Lionel) Messi, wanaweza kufanya hivyo," alisema Lampard.
    "Barcelona hawawezi kutudharau sisi, lakini kuwafunga Tottenham si onyo kwao. Wametengeneza timu waliyonayo.
    "Wazi ni changamoto kubwa ambayo sijawahi kukutana nayo,”alisema.
    Ikiwa na Muargentina, Messi anayeogelea kwenye moja ya misimu ya mafanikio makubwa katika historia ya soka, ni wazi ndiye anayetia ganzi matumaini ya Chelsea kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya pili.
    Na Lampard amesema Messi amempiku hata Muargentina mwenzake Diego Maradona kama mchezaji bora daima kuwahi kutokea.
    "Amekuwa bora zaidi tangu tumecheza nao mwaka 2009 na alikuwa mchezaji mzuri wakati huo.
    Kiwango alichofikia kisoka ni kitu ambacho sijawahi kuona kabla," alisema Lampard.
    "Nimekuwa wakati wa Maradona. Alikuwa kioo change na nafikiri Messi amevuka kiwango chake.
    "Kukaribia mabao 70 ni wazimu. Anastahili. Ni mchezaji bora duniani."
    Lakini licha ya kuwatukuza nyota wa Barca na staili yao ya kucheza, Lampard amesema hivi karibuni Chelsea imezinduka chini ya kocha Roberto Di Matteo na kuonyesha kwamba wanaweza kuwatia misukosuko mabingwa hao wa Hispania.
    "kama tutacheza kama tulivyocheza leo (dhidi ya Spurs) kwa kujituma na nguvu tuliyonayo kwenye timu, tunatakiuwa kuamini tuna nafasi," alisema Lampard.
    "Tupo kwenye Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa. Hatuwezi kuonyesha woga sana dhidi yao. Tunatakiwa kuwaheshimu, lakini pia kushuka nao uwanjani na kucheza kwa aina yetu.
    "Ninapowaangalia Barcelona, natarajia wao watashinda, lakini unatakiwa kujiamini mwenyewe. Tumewahi kuwapa wakati mgumu kipindi kilichopita na tuko tayari kujaribu kufanya hivyo tena."
    Lampard pia alisema kwamba hakuna mvuto wa ziada kutokana na kipigo walichokipata mwaka 2009 dhidi ya Barca, siku ambayo Chelsea walinyimwa penalti kabla ya Iniesta kufunga bao la ushindi dakika za lala salama na wakafuzu kwa faida ya bao la ugenini.
    "Hiyo kwa kweli haipo tena katika fikra zetu," alisema Lampard. "Wamepiga hatua kutoka miaka mitatu iliyopita nasi tumebadilika pia."
    Lampard na wachezaji wenzake wamebakiza siku mbili tu za kujiandaa kuivaa Barca, lakini nyota huyo wa England mwenye umri wa miaka 33 hana shaka watakuwa tayari baada ya safari ya Spurs.
    "Nafikiri ilikuwa ni ishara nzuri kwa Chelsea katika ubora wetu na watu wanavyofahamu jinsi tulivyuo sasa," Lampard alisema.
    "Tulikuwa wa nguvu Uwanja mzima baada ya kipindi cha kwanza kigumu. Kipindi cha pili kilikuwa kizuri kama tulivyocheza msimu wote. Tuna kikosi kizuri na wote tulikuwapo wakati huo.
    "Kama hauwezi kuchangamsha akili na mwili wako kwa ajili ya Barcelona, sijui wakati gani utafanya. Siwezi kuomba kupumzishwa kwenye mchezo huo kwa kwa kweli!"
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LAMPARD: TUTAKOMAA NAO NA MESSI WAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top