• HABARI MPYA

    Sunday, April 15, 2012

    MAMA KANUMBA ATOA WOSIA

    Mama Kanumba na Asha Baraka kulia
    MAMA Mzazi wa aliyekuwa msanii wa filamu nchini marehemu Steven Kanumba amewataka wasanii wanachama wa Mtandao wa Wasanii Tanzania
    (SHIWATA) kuendeleza ushirikiano alioacha mwanae.
     Akizungumza katika ibada ya kumuombea mwanae iliyoandaliwa na (SHIWATA) leo  Dar es Salaam, Mama Kanumba alisema amefarijika kuona
    wasanii wanaendelea kumuombea mwanae kila kona ya nchi.
    "Nawashukuru SHIWATA kwa moyo wa ipendo na ushirikiano mlionesha kwa familia yangu, naomba muendeleze ushirikiano mliokuwa nao wakati mwanangu akiwa nanyi, endeleeni kushirikiana" alisema Mama Kanumba.
    Katika ibada hiyo iliyoongozwa na mchungaji wa Kanisa la Elim Pentekoste Ilala Bungoni, Mchungaji Livingstone Mwaitela alisema wasanii na familia ya Kanumba wasisononeke kwa sababu Mungu alimpenda mtoto wao huyo zaidi.
     Alisema wasanii waendelee kumkumbuka mwenzao kwa kubadili mambo yasiyompendeza Mungu badala yake wajiandae kwa kufanya mambo ambayo
    yanampendezesha na kujiweka tayari siku akiwaita wawe tayari.
    Mwenyekiti wa SHIWATA,Caasim Taalib alisema Kanumba alikuwa mwanachama wao namba 648 akiwa mmoja wa waliojitokeza kutafuta eneo kwa ajili ya kujenga nyumba za wasanii kutoka Bagamoyo, Kisarawe na hatimaye kufanikiwa kupata eneo Mkuranga.
    Marehemu Kanumba alifariki Aprili 5, wakati akikimbizwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) baada ya kuanguka nyumbani kwake
    Sinza kufuatia ugomvi wa mapenzi na msanii mwenzake Elizabeth Michael (Lulu).
     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAMA KANUMBA ATOA WOSIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top