• HABARI MPYA

    Friday, July 13, 2012

    TUSKER WATUA LEO KUKAMILISHA IDADI TIMU ZA KAGAME 2012


    Kikosin cha Tusker FC

    Na Prince Akbar
    MABINGWA wa zamani Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Tusker ya Kenya na Ports ya Djibouti zinawasili leo jioni kukamilisha idadi ya timu 11 zinazoshiriki mashindano ya Kombe la Kagame yanayoanza kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Mechi za kesho ni APR ya Rwanda dhidi ya El Salam Wau ya Sudan Kusini itakayoanza saa 8 kamili mchana na kufuatiwa na ya saa 10 kamili jioni kati ya mabingwa watetezi Yanga na Atletico ya Burundi.
    Timu zote kutoka nje ya mazoezi zimeshapangiwa viwanja vya mazoezi ambapo zitavitumia kwa mujibu wa ratiba ambayo imepangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Makazi ya timu hizo na viwanja vya mazoezi ni kama ifuatavyo;


    Timu:                   Uwanja wa mazoezi:              Accommodation:
    APR (Rwanda)       Mabibo Hostel                         - Marriott Hotel (Mabibo External)
    AS Vita (Congo)    University of Dar es Salaam     - Chichi Hotel (Kinondoni)
    Atletico (Burundi) Mabibo Hostel                         - Lunch Time Hotel (Mabibo Hostel)
    Azam (Tanzania)   Azam Complex                        - Azam Complex (Chamazi)
    El Salam Wau (S. Sudan) Zanaki Sekondari           - Rungwe Hotel (Kariakoo)
    Mafunzo (Z’bar)    Kinesi                                     - Rombo Green View Hotel (Sinza)
    Ports (Djibouti)     Kinesi                                     - Rombo Green View Hotel (Sinza)
    Simba (Tanzania)  …………………….                         – Vina Hotel (Mabibo Makutano)
    Tusker (Kenya)     Zanaki Sekondari                     - Rungwe Hotel (Kariakoo)
    URA (Uganda)       Loyola                                     - Valentino Royal Hotel (Kariakoo)
    Yanga (Tanzania)  ………………….                            – ……………………….
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TUSKER WATUA LEO KUKAMILISHA IDADI TIMU ZA KAGAME 2012 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top