• HABARI MPYA

    Thursday, August 16, 2012

    MECKY MEXIME ASEMA WATOTO WA SIMBA HAWAMNYIMI USINGIZI

    Mecky Mexime

    Na Princess Asia
    KOCHA wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Mecky Mexime amesema kwamba ana matumaini ya kuwafunga Simba B na kubeba na Kombe la Bank ABC katika fainali itayapopigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, Mecky alisema kwamba amewaona Simba wakati wanaitoa Azam kwa kuichapa 2-1 ni wazuri na wanacheza kwa uelewano sana, lakini Jumamosi anaamini atawafunga tu.
    “Kabla sijawa kocha wa Mtibwa ya wakubwa, nilikuwa kocha wa vijana, na nilikuwa pia kocha wa vijana wa Morogoro katika Copa Coca Cola, ambayo ilikchukuja ubingwa. Kwa hiyo nawajua vijana, hivyo vijana wa Simba hawanipi hofu,”alisema Mecky.
    Mexime alisema anajua namna ya kuwapoteza vijana uwanjani na kuvuna ushindi, tena wa mabao ya kutosha kabisa,  
    Mtibwa Sugar ilitinga Fainali kwa kishindo, kwa kuinyuka Jamhuri ya Pemba, mabao 5-1, ambayo yalitiwa kimiani na Babu Ally Seif dakika ya 15, Salvartoy Ntebe dakika ya 17, Mfaume Shaaban aliyejifunga dakika ya 38, Vincent Barnabas dakika ya 43 na Awadh Juma dakika ya 85 wakati la kufutia machozi la Jamhuri lilifungwa na Mbarouk Chande dakika ya 62.
    Hadi sasa, Mtibwa ndio timu pekee ambayo haijapoteza pointi hata moja kwenye mashindano hayo baada ya kushinda mechi zake zote tatu za Kundi B, 2-1 dhidi ya Polisi Moro, 2-0 dhidi ya Azam na 5-0 dhidi ya Super Falcon na jana 5-1 dhidi ya Jamhuri katika Nusu Fainali.
    Simba B yenyewe ilitoa sare moja tu ya kufungana 1-1 na Jamhuri katika mchezo wa kwanza, lakini mechi zake nyingine ilizifunga 2-0 kila timu, Mtende na Zimamoto ya Zanzibar.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECKY MEXIME ASEMA WATOTO WA SIMBA HAWAMNYIMI USINGIZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top