Mashabiki
wa soka nchini Rwanda wameonyesha ni kiasi wanaipenda Yanga baada ya jana
kugombana wakiwania jezi za klabu hiyo, iliyokuwa ziarani nchini humo. Patashika
hiyo ya nguo kuchanika kuwania jezi za mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati
ilitokea wakati wa mapumziko ya mchezo kati yao na Polisi, Uwanja wa Amahoro. Yanga
ilikuwa Kigali tangu Jumanne iliyopita, kwa ziara ya michezo ya kirafiki na
ikiwa huko, ilimtembelea rais Kagame Ikulu na pia kuzuru katika makaburi ya
kumbukumbu ya mauaji ya Rwanda wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Katika mechi
zake, Yanga, inayorejea leo Dar es Salaam iliifunga Rayon 2-0 Ijumaa na jana Polisi
2-1. Tazama picha hizi, zilizopigwa na Saleh Ally, Mhariri kiongozi gazeti la
Championi jinsi watu walivyogombea jezi za Yanga.
Hodgkinson eases to victory in 800m heat
-
Great Britain's Keely Hodgkinson wins her 800m heat to ease into the
semi-finals of the women's 800m at the World Athletics Championships in
Tokyo.
15 minutes ago
0 comments:
Post a Comment