![]() |
Lulu |
SIKU chache baada ya kufikishwa
mahakamani kwa msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael 'Lulu' kwa tuhuma za
kuhusika na kifo cha msanii mwenzake Steven Kanumba, waislamu wamelaani msanii
huyo kutoka mahakamani akiwa amevalia vazi la Hijab.
Kwa mujibu wa mamapipiro blogspot, tamko hilo lililotolewa jana
katika msikiti wa Ngazija jijini Dar es Salaam wakati wa Swala ya Ijumaa ambapo
waumini hao walidai kuwa msanii huyo anaudhalilisha uislamu.
Walisema hawakupendezwa na
kitendo hicho na kama atapandishwa tena mahakamani katika mavazi hayo wataandamana.
0 comments:
Post a Comment