• HABARI MPYA

    Thursday, March 14, 2013

    ARSENAL YAFA KIUME ULAYA, BAYERN YAPIGWA 2-0 MUNICH


    Aaron Ramsey
    KLABU ya Arsenal imetolewa kiume katika Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu baada ya kushinda 2-0 ugenini dhidi ya Bayern Munich nchini Ujerumani.
    Matokeo hayo yanamaanisha matokeo ya jumla ni 3-3 baada ya awali, Bayern kushinda 3-1 Jijini London.
    Bayern imesonga mbele kwa faida ya mabao ya ugenini na sasa imejikita Robo Fainali.
    Olivier Giroud aliifungia Arsenal bao la kwanza dakika ya tatu ambalo lilidumu hadi mapumziko. 
    Laurent Koscielny akaja kuwafungia la pili The Gunners dakika ya 86, lakini Bayern wakabebwa na mabao yao ya ugenini kusonga mbele. 

    VIKOSI;

    Bayern Munich: Neuer, Dante, Van Buyten, Lahm, Martinez, Muller, Alaba, Dias, Kroos/Tymoschuk dk81, Mandzukic/Gomez dk73, Robben
    Benchi: Tom Starke, Rafinha, Contento, Shaqiri, Pizarro
    Kadi za njano: Lahm, Martinez, Gomez

    Arsenal: Fabianski, Mertesacker, Koscielny, Jenkinson, Gibbs, Rosicky, Arteta, Walcott/Oxlade-Chamberlain dk72, Ramsey/Gervinho dk72, Cazorla, Giroud
    Benchi: Mannone, Vermaelen, Diaby, Coquelin, Arshavin
    Kadi za njano: Gibbs, Rosicky, Giroud, Mertesacker, Cazorla, Koscielny
    Wafungaji wa mabao: Giroud dk3 na Koscielny dk86
    Refa: Pavel Kralovec
    Mahudhurio: 66,000

    Close: Laurent Koscielny scored late in the match to set up a tense finish
    Laurent Koscielny akifunga bao la pili kwa kichwa dakika za mwishoni
    Fracas: Goalkeeper Manuel Neuer tries to hold onto the ball to buy some time for Bayern
    Kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer akiuzuia mpira dhidi ya wachezaji wa Arsenal baada ya kufungwa bao la pili, ili kupoteza muda
    Game on: Olivier Giroud scored early in the match to put pressure on the German hosts
    Olivier Giroud akifunga bao la mapema lililowatia presha wenyeji
    Booked: Thomas Rosicky looks dejected after a heavy tackle on Arjen Robben
    Thomas Rosicky akionekana mwenye hasira baada ya kupewa kadi ya njano kwa kumchezea rafu Arjen Robben
    Sliding in: Javi Martinez (right) tries to nick the ball away from Mikel Arteta
    Javi Martinez (kulia) akiondosha mpira miguuni mwa Mikel Arteta.
    Frustrated: Mario Mandzukic shows his disappointment at a refereeing decision
    Mario Mandzukic akilalamikia uamuzi wa refa
    Remonstrating: Arsene Wenge rages at the fourth official
    Arsene Wenger akizozana na refa wa akiba
    Seething: Wenger screams from the touchline after another decision
    Wenger akikaribia mstari wa kuingia uwanjani huku akilalamikia uamuzi wa refa.
    Digging deep: Luis Gustavo (right) tries to dispossess Santi Cazorla in the middle of the park
    Luis Gustavo (kulia) akijaribu kumdhibiti Santi Cazorla
    Big shout: Thomas Muller screams at the referee's assistant during the first half of the tie
    Thomas Muller akimbwatukia mshika kibendera
    Rough and tumble: Arjen Robben is sent flying as Kieran Gibbs slides in
    Arjen Robben akienda chini baada ya kupitiwa na kwanja la Kieran Gibbs
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ARSENAL YAFA KIUME ULAYA, BAYERN YAPIGWA 2-0 MUNICH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top