• HABARI MPYA

    Sunday, April 15, 2012

    MESSI AMKAMATA RONALDO, BARCA, REAL ZOTE ZAUA LA LIGA

    Messi
    MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Lionel Messi amefunga bao la penalti dhidi ya Levante usiku huu na kufikia rekodi ya Cristiano Ronaldo katika Ligi Kuu ya Hispania ya kufunga mabao 41 msimu mmoja, aliyoiweka saa chache kabla.
    Messi alitumbukiza mkwaju wake wa penalti dakika ya 72 na kuipa Barcelona ushindi wa 2-1 na kumfikia Ronaldo, ambaye aliweka rekodi hiyo kwa bao la dakika ya 74 la kichwa katika ushindi wa Real Madrid wa 3-1 dhidi ya Sporting Gijon.
    Madrid imeendelea kuongoza La Liga kwa tofauti ya pointi nne dhidi ya mabingwa watetezi mara tatu, Barcelona kabla ya mechi baina ya timu hizo, maarufu kama El Clasico wiki ijayo, ambayo itatoa picha yam bio za ubingwa msimu huu zikiwa zimebaki mechi nne ligi kufikia tamati.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AMKAMATA RONALDO, BARCA, REAL ZOTE ZAUA LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top