![]() |
Rosicky kushoto na Alex Song |
NYOTA wa Arsenal Tomas Rosicky amesema
kwamba tayari sasa wameungana na mashabiki wao kwenye Uwanja wa Emirates na
wamejenga imani.
Kwa ujumla, Arsenal imekuwa
ikifanya vizuri katika mechi za nyumbani msimu huu, ikiwa imepoteza mechi tatu
tu katika mashindano yote na na kufunga mabao 24 katika mechi zao saba
zilizopita.
Rosicky anaamini mashabiki
wamechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio hayo na kiwango kizuri cha Arsenal na
anaamini kwa pamoja wanaweza kufanya Emirates iwe kiota chao cha shangwe.
“Siku za karibuni mapokeo yamekuwa
mazuri katika mechi zetu za nyumbani – timu inayoweza kuhisi hilo na ni msaada
mkubwa kwetu,”alisema.
“Ni hisia nzuri kuwa na
mashabiki ambao wako nyuma yako kwa dakika zote 90.
“Kwa kweli mashabiki wanatufanya
tufanye tofauti kwenye Uwanja wa Emirates na tunatumai tutadumisha muungano huu
kwa kuendeleza wimbi la ushindi zaidi.”
0 comments:
Post a Comment