• HABARI MPYA

    Sunday, April 15, 2012

    FERGUSON AMTOA KWA MKOPO FABIO

    Fabio
    KOCHA Sir Alex Ferguson amesema kwamba Fabio atatolewa kwa mkopo msimu ujao.
    Beki huyo wa Kibrazil mara kadhaa amekuwa akipelekwa kikosi cha wachezaji wa akiba msimu huu katika siku za karibuni, lakini amecheza mechi moja tu ya Ligi Kuu England, tena akiingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Patrice Evra katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Wolves.
    Kocha anahofia kijana huyo mwenye umri wa miaka 21 anahitaji uhakika wa kucheza katika umri wake mdogo na yuko tayari kumpeleka klabu nyingine kwa msimu wa 2012/2013.
    Baada ya kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Barcelona msimu uliopita, beki huyo wa pembeni amecheza mechi 15 tu msimu huu,  nyingi kati ya hizo zikiwa za Ulaya au Kombe la Ligi.
    "Natumai kwamba Fabio ataendelea vema kama pacha wake [Rafael] na, kumsaidia, atakwenda kucheza kwa mkopo msimu ujao kumpa uzoefu wa kucheza kikosi cha kwanza," alisema kocha katika safu yake maalum leo.
    "Tayari nimekwishazungumza naye na anatambua thamani ya kucheza kwa uhakika katika kiwango cha juu, kuliko nafasi ambayo tunampa hivi sasa."
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FERGUSON AMTOA KWA MKOPO FABIO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top