Published: Today at 11:35
FAMILIA ya nyota mweusi wa kikosi cha timu ya taifa soka ya England, Theo Walcott haitakwenda kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya, Euro 2012 mwezi ujao kwa sababu wanahofia usalama wao.
Kaka wa winga huyo Arsenal, Ashley hawatahatarisha maisha yao kwa kwenda Ukraine kumuangalia ndugu yao, nyota wa England, Theo mwenye umri wa miaka 23, jana alitajwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo cha Roy Hodgson.
Nyota huyo alifanyiwa kejeli za kibaguzi, akionyeshwa ishara ya nyani kwa pamoja na mchezaji mwenzake wa England na mashabiki wa Ubelgiji katika michezo ya awali Ulaya Mashariki Septemba mwaka jana.
UBAGUZI
Jana Ashley aliandika kwenye Twitter akisema kwamba yeye na baba yake Theo, Don watabaki mbali kabisa na Ukraine - na Ashley anahoji busara ya kupeleka mashindano katika nchi ambayo mashabiki hawatakuwa salama.
Aliandika: “Kwa bahati mbaya, baba yangu na mimi tumeamua kutosafiri kwenda Ukraine kwa sababu ya kuihofia mashambulizi ya kibaguzi.
0 comments:
Post a Comment