Published: Today at 00:59
JOHN TERRY si pekee aliyesherehekea taji la ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya la Chelsea – Rihanna pia.
Mwimbaji huyo wa Bajan aliungana na wachezaji wa Blues katika pati la ubingwa usiku.
Aliwasili klabu la West End, Boujis baada ya kuachana na Jay-Z na Kanye West usiku huo wakiwa kwenye tamasha.
Alikimbilia kwenye pati la wachezaji na alipofika tu akamvaa Didier Drogba — ambaye penalti ya mwisho iliimaliza Bayern Munich nchini Ujerumani Jumamosi. Chanzo kilisema: “Rihanna alimfuata Didier, Jose Bosingwa, Salomon Kalou, Michael Essien na Raul Meireles na wakatengenza mduara kwenye meza yao.
“Wachezaji walifurahia kukutana naye, lakini alikuwa karibu zaidi na Didier na alikuwa akicheza naye.”
Baadaye aka- tweet picha aliyopiga na mshambuliaji huyoa akiiandikia: “THEE DIDIER DROGBA #thereisaGod.” Lakini hakuwa mwanamke pekee aliyefurahia pati la Chelsea.
Christine Bleakley aliungana na mpenzi wake Frank Lampard, John Obi Mikel na Carlton Cole katika klabu ya Mayfair, Aura.
0 comments:
Post a Comment