• HABARI MPYA

    Thursday, May 17, 2012

    SAMATTA ANUSURIKA KUFA AJALINI, AAMUA KUWA SALA TANO


    Mbwana Samatta

    MSHAMBULIAJI chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amenusurika kufa kwa ajali ya gari leo mjini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    Samatta anayechezea Tout Puissant Mazembe, ameiambia BIN ZUBEIRY leo mchana kwamba alikoswakoswa na gari la abiria leo asubuhi.
    “Nipeni pole na mie, maana nimekoswa koswa leo asubuhi na gari ya abiria, sidhani kama ningeomba hata maji,”alisema.
    Aidha, Samatta amesema baada ya kunusurika na kifo, kuanzi leo atakuwa anasali sala tano. “Kuanzia leo, nitakuwa wa kwanza masjid,”alisema.
    Samatta pia amesikitishwa na kifo cha kiungo wa Simba, Patrick Mutesa Mafisango na amewapa pole wapenzi wa SImba na familia ya marehemu.
    Samatta ameiambia BIN ZUBEIRY kutoka Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kifo hicho kimesmshitua sana, lakini hana budi kukubali kwa kuwa ni kazi ya Mungu.
    “Dah majonzi tena, poleni familia ya Patrick Mutesa, poleni Simba SC, poleni wapenzi wa soka Tanzania, hatuna jinsi, Mungu ndio mpangaji wa yote,”alisema.
    Mafisango alifariki dunia usiku wa kuamkia leo, eneo la Tazara, Dar es Salaam kwa ajali ya gari.
    Vyanzo vimesema alikuwa anatoka Maisha Club disko na akiwa katika eneo hilo alikutana na mwendesha pikipiki aliyeingia ovyo na katika kumkwepa alijikuta anatoka barabarani na kuingia mtaroni na kupoteza maisha.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA ANUSURIKA KUFA AJALINI, AAMUA KUWA SALA TANO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top