Published: Today at 01:11
WACHEZAJI wa timu ya soka ya taifa ya England, watakwenda kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya, Euro 2012 bila chupi.
Hiyo ni kwa sababu Chama cha Soka England (FA) kitawapa wachezaji wote wa Roy Hodgson vifaa vyote ikiwemo chupi za timu.
Kipa namba moja wa Norwich, John Ruddy, aliyeongea na Hodgson, alisema: “Nimeambiwa na nichukue viatu, glavu, vifaa vya mazoezi, na nguo chache za kawaida na karatasi (za choo). Ninafurahi kila kitu kitakuwa kimeandaliwa kwa ajili yangu huko.
“Tumepata suti na wanaandaa chupi kwa ajili yetu. Ni kweli, lakini hiyo ndio faida ya kuwa katika kikosi cha England.
Nguo hizo zitasambazwa na kampuni ya M&S, wakati England itaweka kambi yake katika hoteli ya katikati ya jiji, Krakow, Poland.
Hapo ni jirani na kambi ya jeshi la Vita Kuu ya Pili ya Dunia, Nazi, Auschwitz na FA imempanga kutembelea na wachezaji.
0 comments:
Post a Comment