• HABARI MPYA

    Wednesday, December 05, 2012

    CANNAVARO: KENYA WAUPE, TUTAWANG'OA WATAKE WASITAKE

    Cannavaro

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    NAHODHA wa Zanzibar, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ alikuwapo jana Uwanja wa Mandela, Namboole akiishuhudia Kenya ikiichapa Malawi 2-0 na kutinga Fainali, lakini amesema Harambee Stars ‘weupe tu kwao’.
    Akizungumza jana baada ya mechi hiyo, Cannavaro alisema kwamba kulingana na kiwango kiliochoonyeshwa na Kenya katika mechi hiyo dhidi ya Malawi, wanaamini watawafunga.
    “Yaani jamaa weupe sana, hata bao walilopata la kibahati bahati sana, mimi nakuambia sisi hawa tunawafunga, timu yetu nzuri sana,”alisema beki huyo wa kati wa Yanga SC ya Dar es Salaam.
    Nahodha huyo wa Yanga SC, alisema kwamba baada ya kuitoa Burundi juzi sasa anaamini Kombe la Challenge litakwenda Zanzibar, kwani haoni timu nyingine ya kuwasumbua wao katika mashindano haya.
    Zanzibar juzi ilikata tiketi ya kutinga Nusu Fainali baada ya kuichapa Burundi kwa penalti 6-5 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 na sasa itacheza na mshindi kati ya Kenya na Malawi katika Nusu Fainali.
    Shujaa wa Zanzibar juzi alikuwa ni Abdallah Othman aliyefunga penalti ya mwisho, baada ya kipa Mwadini Ally kupangua penalti ya Abdul Fiston wa Burundi.
    Manahodha wa timu zote, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Zanzibar na Suleiman Ndikumana wa Burundi walipoteza penalti zao juzi.
    Ndikumana alikuwa wa kwanza kwenda kupiga na mkwaju wake ukaota mbawa na kupaa juu ya lango, wakati wenzake waliofunga mbali na Fiston kupoteza ni Steve Nzigamasabo, Amisi Tambwe, Chris Nduwarugira, Leopold Nkurinkiye na Gael Duhatindavyi.
    Upande wa Zanzibar Heroes, Khamis Mcha ‘Vialli’ alikwenda kufunga penalti ya kwanza ya Zanzibar, Adeyom Saleh Mohamed akafunga ya pili, Jaku Juma akafunga ya tatu, kabla ya Cannavaro kumpelekea mikononi mkwaju wake kipa Arthur Arakaza wa Burundi, Samir Hajji Nuhu akafunga ya tano, Aggrey Morris akafunga ya sita na Othman kutumbukiza nyavuni ya ushindi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: CANNAVARO: KENYA WAUPE, TUTAWANG'OA WATAKE WASITAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top