• HABARI MPYA

    Tuesday, December 04, 2012

    STARS NA UGANDA NUSU FAINALI TUSKER CHALLENGE 2012

    Wachezaji wa Uganda wakimpongeza Geoffrey Kizito (anayetazama kamera amekumbatiana na Kiiza), baada ya kufunga bao kwanza dakika ya nne dhidi ya Ethiopia katika Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala. Uganda ilishinda 2-0 bao lingine likifungwa na Robert Ssentongo dakika ya 60 na kwa ushindi huo, Uganda itamenyana na Tanzania Bara katika Nusu Fainali Alhamisi usiku, mchezo ambao utatanguliwa na Nusu Fainali nyingine kati ya Kenya na Zanzibar.
    Ssentongo akisababisha

    Kiiza mawindoni

    Kipa Samson Asfaw Worku akiwa amedaka mpira, huku beki wake Girma Bekele Debele akimdhibiti Brian Umony kulia

    Gotochi Panom Yietch akigombea mpira na Robert Ssentongo kulia

    Robert Ssentongo anaondoka na mpira baada ya kumlamba chenga beki wa Ethiopia kulia

    Hamisi Kiiza akimtoka Chala Deriba Debala wa Ethiopia

    Kiiza, Walusimbi, Wasswa wakicheza na Ssentongo 

    Kutoka kulia Hamisi Kiiza na Henry Kalungi wakimpongeza Robert Ssentongo kufunga bao la pili

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: STARS NA UGANDA NUSU FAINALI TUSKER CHALLENGE 2012 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top