• HABARI MPYA

    Wednesday, December 19, 2012

    UCHAGUZI TWFA LEO MORO

    Kila heri mdau Zena Chande 'Zen C'

    Na Princess Asia
    UCHAGUZI wa viongozi wapya wa Chama cha Soka ya Wanawake Tanzania (TWFA) unafanyika leo kwenye hoteli ya Midlands mjini Morogoro.
    Kamati ya Uchaguzi ya TWFA ikiongozwa na Mama Ombeni Zavala ndiyo itakayoendesha uchaguzi huo chini ya usimamizi wa Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
    Wagombea katika uchaguzi huo ni Isabela Kapera, Joan Minja na Lina Kessy wanaowania uenyekiti, Rose Kissiwa (mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti), Amina Karuma na Cecilia Mkafum (wanawania ukatibu mkuu).
    Wengine ni Zena Chande (mgombea pekee wa nafasi ya Mjumbe Mkutano Mkuu wa TFF) na Sophia Charles na Triphonia Temba wanaowania ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: UCHAGUZI TWFA LEO MORO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top