• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    GIUSEPPE ROSSI AUMIA TENA MASIKINI

    Rossi
    KLABU ya Villarreal imesema mshambuliaji Giuseppe Rossi ameumia tena goti lake la mguu wa kulia na atakuwa nje ya Uwanja kwa miezi sita zaidi, na kupoteza matumaini ya kuichezea Itali katika Kombe la Mataifa Ulaya.
    Rossi aliumia mguu wake katika mechi dhidi ya Real Madrid, Oktoba 26 na kufanyiwa upasuaji.
    Villarrreal imesema Rossi ameumia tena mguu wake katika mazoezi leo na anahitaji upasauji mwingine.
    Ataukosa mwanzo wa msimu ujao.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ameifungia mabao 32 Villarreal katika mashindano yote msimu uliopita.
    Raia huyo wa new Jersey, mtoto wa Wataliano, aliamua kuichezea The Azzurri badala ya Marekani na amefunga mabao sita katika mechi 27 za kimataifa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GIUSEPPE ROSSI AUMIA TENA MASIKINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top