• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI JANGWANI


    THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

    DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS



    Telephone: 255-22-2114512, 2116898
                  press@ikulu.go.tz             

    Fax: 255-22-2113425


    PRESIDENT’S OFFICE,
          THE STATE HOUSE,
                  P.O. BOX 9120,  
    DAR ES SALAAM.
    Tanzania.
     

    TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

    RAMBIRAMBI

    Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti  wa klabu ya mpira wa miguu ya Young Africans Sports Club (Yanga)  Bw. Lyod Nchunga kufuatia kifo cha Mjumbe wake wa Kamati ya Utendaji, wakili Theonist Rutashoborwa, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kutokana na ugonjwa wa Shinikizo la Damu na Kisukari.

    “Nimepokea kwa Masikitiko na huzuni sana taarifa za wakili Theonist Rutashoborwa kilichotokea usiku wa Kuamkia leo, hili ni pigo na pengo kubwa katika klabu ya Yanga katika kipindi hiki cha kushiriki ligi kuu” Rais amesema.

    “Naomba unifikishie rambirambi zangu za dhati kwa familia, wachezaji na wana Yanga wote kwa kuondokewa na Mjumbe wao katika kipindi hiki” Rais ameongeza na kuwataka wana Yanga wawe wavumilivu wakati wa msiba huu na kumuombea Bw. Rutashoborwa mapumziko mema ya Milele.

    ……………Mwisho…………



    Imetolewa na Premi Kibanga,

    Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi.

    Ikulu-Dar-Es-Salaam

    12 April, 2012
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI JANGWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top