• HABARI MPYA

    Monday, April 16, 2012

    ROONEY, VAN PERSIE WACHONGANISHWA PFA, NANI ATAIBUKA KIDUME?

    Van Persie
    Rooney na Wellbeck
    MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Robin van Persie ni miongoni mwa wachezaji sita walioingizwa kwenye kinyang’anyiro cha Chama cha Wachezaji wa Kulipwa England, PFA katika Ligi Kuu msimu.
    Nahodha huyo Arsenal amekuwa na msimu mzuri akifunga mabao ya kutosha, hadi sasa akiwa ametikisa nyavu mara 27 katika ligi na kutoa pasi za mabao 10 kwa wachezaji wenzake.
    Alex Oxlade-Chamberlain, wakati huo huo ameingizwa kwenye kipengele cha kuwania tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka.
    Mshindi wa tuzo hizo anatarajiwa kutajwa Jumapili.
    Orodha ya wanaowania tuzo Mchezaji Bora wa Mwaka wa PFA: Robin van Persie (Arsenal), Wayne Rooney (Manchester United), Scott Parker (Tottenham), Sergio Aguero, Joe Hart, David Silva (wote Manchester City).
    Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka PFA: Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Gareth Bale, Kyle Walker (both Tottenham), Danny Welbeck (Manchester United), Sergio Aguero (Manchester City), Daniel Sturridge (Chelsea).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ROONEY, VAN PERSIE WACHONGANISHWA PFA, NANI ATAIBUKA KIDUME? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top