![]() |
Kolo na mkewe mtarajiwa |
BEKI wa Manchester City, Kolo Toure anatarajia kufunga pingu
za maisha na mpenzi wake wa siku nyingi na mama wa watoto wake wawili, Chimene
Akassou Juni 16 na 17 nchini Ivory Coast, amesema mchezaji huyo katika taarifa
yake bongostaz.blogspot.com leo.
Wawili hao wamekuwa wakiishi pamoja England tangu mwaka
2003, mwaka mmoja tu tangu mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ivory Coast ajiunge
na Arsenal, akitokea klabu yake iliyomuinua nchini mwao, Asec Mimosas.Baada ya kufunga ndoa Mairie de Cocody mjini Abidjan, sherehe zitaendelea kanisani na msikitni, imesema taarifa hiyo.
Toure, mwenye umri wa miaka 31, ni muumini wa dini ya Kiislamu, wakati mkewe mtarajiwa ni Mkristo.
Ni miongoni mwa wachezaji wenye mafanikio makubwa katika nyota wa Ivory Coast na amecheza Fainali tatu za Kombe la Mataifa ya Afrika na mbili za Kombe la Dunia.
Machi mwaka 2011 alikutwa na hatia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu zilizopigwa marufuku michezoni na akatumikia adhabu ya kusimama kucheza soka kwa miezi sita.
Ni kaka wa Mwansoka Bora Afrika na mchezaji mwenzake katika timu ya taifa na klabu ya Manchester City, Yaya Toure, na kaka wa mshambuliaji wa zamani wa OGC Nice, Ibrahim Toure.
Nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba alimuoa rasmi mama wa watoto wake watatu, Lalla mwaka jana mjini Monaco, Ufaransa.
0 comments:
Post a Comment