• HABARI MPYA

    Saturday, August 11, 2012

    MASWALI SITA YA KUJIULIZA KUHUSU SIMBA SC NA MAMBO YAO LEO

    Lino Masombo kushoto, akimpongeza Juma Kaseja baada ya fainali ya Kombe la Urafiki, ambayo Simba iliifunga Azam FC kwa penalti, baada ya sare ya 2-2. 


    Na Mahmoud Zubeiry
    1.                      Kwa nini habari zilivuja Mwenyekiti wa Simba SC alimpa Mbuyu Twite dola za Kimarekani 30,000, wakati sasa inaelezwa mchezaji huyo alipewa dola 10,000 tu

    2.                      Simba ilisema ilimuongezea mkataba Kevin Yondan, je ilimpa na fedha? Na kama ilimpa fedha mbona hazijavuja habari zozote juu ya fedha alizopewa, wakati inajulikana hadi Felix Sunzu analipwa dola za Kimarekani 3,500 kwa mwezi?

    3.                      Simba ilimsajili na kumpa fedha beki Lino Masombo kutoka DRC, tena inaelezwa ni fedha nyingi tu, je baada ya kumtema bila kumpa muda wa kutosha kujiridhisha kuhusu uwezo wake (mdogo au mkubwa), ili kukwepa kurudia makosa yaliyofanyika katika kumtema Derrick Walullya, fedha hizo zinarudishwa au?

    4.                      Ukitazama kikosi cha Simba kwa sasa utagundua wamesheheni viungo kibao, Amri Kiemba, Jonas Mkude, Christopher Edward, Mussa Mudde, Haruna Moshi, Kanu Mbivayanga, Mwinyi Kazimoto, Uhuru Suleiman, Kiggi Makassy, Salim Kinje, Ramadhan Singano ‘Messi’, Mrisho Ngassa na Ramadhan Chombo ‘Redondo’, wakati mabeki wa kati ni Juma Nyosso, Shomary Kapombe na Obadia Mungusa, (Zingatia, kiasili Kapombe na Maftah kiasili ni viungo) je, hii iko sawa?

    5.                      Nani huwa anashauri masuala ya usajili ndani ya Simba…Kusajiliwa au kukatwa kwa mchezaji, je anafanya kazi yake vizuri?   

    6.                      Kitaalamu inafahamika, kumchezesha mchezaji mechi, kabla hajawa fiti kwa angalau zaidi ya asilimia 50 ni kumtengenezea mazingira ya kuumia na tumeshuhudia majeruhi wengi katika siku za karibuni Simba SC, je kwa nini Kocha Mkuu, Mserbia Milovan Cirkovick anaruhusu hali hii? 
    NANI MSHAURI WAO; Benchi la Ufundi Simba SC kutoka kushoto Kocha Mkuu, Milovan Cirkovick (Serbia), Msaidizi Hamatre Rochard (Uganda) na Kocha wa makipa, Mzalendo, James Kisaka.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MASWALI SITA YA KUJIULIZA KUHUSU SIMBA SC NA MAMBO YAO LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top