• HABARI MPYA

    Friday, August 10, 2012

    STARS YAANZA VEMA MAANDALIZI YA KUIVAA BOTSWANA

    Juma Kaseja mazoezini


    John Bocco kulia, nyuma yake ni kocha Poulsen

    Bocco kulia na Poulsen 

    Bahanuzi na Boban kulia

    Ngassa na Bahanuzi kulia

    Bocco na Boban kujia

    Ngassa na Nyoni 

    Kocha wa makipa Juma Pondamali kulia, akiwaongoza makipa Kaseja, Dida na Mwadini
    TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars leo imeanza maandalizi ya mchezo wake wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Botswana utakaochezwa Jumatano ijayo mjini Gaborone.
    BIN ZUBEIRY ilitembelea Uwanja wa Karume jioni ya leo, na kuwakuta wachezaji wa timu hiyo wakijifua chini ya walimu wao, Mdenmark Kim Poulsen na wasaidizi wake Sylvester Marsh na Juma Pondamali.
    Wachezaji waliokuwapo mazoezini ni makipa Deogratias Munishi (Azam), nahodha Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni nahodha msaidizi Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba).
    Viungo ni Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi (Simba), Mrisho Ngassa (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Salum Abubakar (Azam) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).
    Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Said Bahanuzi (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC).
    Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, itaondoka Dar es Salaam Jumanne. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STARS YAANZA VEMA MAANDALIZI YA KUIVAA BOTSWANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top